Wednesday 3 September 2014

GARI LA RAIS WA KENYA LAPATIKANA UGANDA



Kenyan presidential security escort President Uhuru Kenyatta's car - March 2013
Magari ya msafara wa Rais yanatakiwa kuwa na ulinzi wa hali ya juu


Gari lililotekwa ambalo ni mali ya idara ya usalama ya Rais wa Kenya limepatikana nchini Uganda.

Gari hilo aina ya BMW lilitekwa Jumatano iliyopita mjini Nairobi huku watekaji wakimtishia dereva kumpiga risasi.

Mkurugenzi wa Interpol Uganda, Assan Kasingye, ameaimbia BBC gari hilo litarejeshwa Nairobi.

Takwimu za hivi karibuni za polisi nchini Kenya zinaonyesha kuwa takriban matukio matatu ya utekaji magari hutokea kwenye mji mkuu wa nchi hiyo.

Mwandishi wa BBC Paul Nabiswa amesema taarifa za tukio hilo zilisambaa kwenye vyombo mbalimbali vya habari nchini Kenya, licha ya msemaji wa Rais Uhuru Kenyatta kujaribu kupunguza makali.

Msemaji huyo alisema gari hilo halikuwa katika msafara wa Rais kwa wakati huo na lilikuwa tu gari la polisi.

Lakini magazeti ya Kenya yameeleza kuwa lilikuwa likiendeshwa na Inspekta wa polisi ambaye ni miongoni mwa maafisa wa usalama wa Rais, amesema mwandishi wa BBC.

Inspekta huyo alivamiwa na watu wanne wenye silaha ambao walimlazimisha kukaa nyuma ya gari na kutimka nalo, gazeti la Kenya Nation lilisema.

Aliachwa nje ya taasisi ya mafunzo ya polisi kwenye wilaya moja mashariki mwa Nairobi saa sita baadae, inaeleza.

Vyombo vya habari vya Kenya vilisema takriban watu watatu wameshakamatwa wakihusishwa na wizi huo Nairobi, kaskazini- magharibi mwa mji mkuu wa nchi hiyo, na Bungoma, mji ulio mpakani na Uganda.


No comments:

Post a Comment