Wednesday 3 September 2014

MWANAMKE WA KWANZA KUTANGAZA BBC DIRA YA DUNIA TV

Mtangazaji wa BBC Idhaa ya Kiswahili Zuhura Yunus amekuwa mwanamke wa kwanza kutangaza kipindi cha BBC Dira ya Dunia Tv kinachorusha matangazo yake kutoka jijini London.

Kipindi cha Dira ya Dunia ya BBC kilianzishwa miaka miwili iliyopita na watazamaji wake wakizoea kutazama sura za watangazaji wa kiume kama Salim Kikeke, Charles Hillary, Peter Musembi na Kassim Kayira .

 Lakini, Septemba 1, 2014, Zuhura Yunus alitangaza kwa mara ya kwanza kwenye kipindi hicho maarufu Afrika Mashariki na wazungumzaji wa Kiswahili duniani kote.

Bi Yunus ambaye ni mtangazaji wa BBC Swahili kwa muda mrefu sasa, ameungana na wafanyakazi wenzake kurusha matangazo ya Dira ya Dunia.

Hongera Bi Zuhura Yunus.

Chanzo: taarifa.co.tz

No comments:

Post a Comment